KEKI RAHISI
Vipimo
Siagi Kikombe 1
Sukari Kikombe
1
Unga Vikombe 2
Maziwa
1/2 (nusu) Kikombe
Mayai 4
Baking Powder 1 Kijiko
cha supu
Arki
rose kidogo
Tupike
Sote sasa
1.
Washa mkaa wako au kama unatumia oveni 350 - 400 Deg C liache lishike moto huku
ukitayarisha mchanganyiko wa keki.
2.
Changanya sukari na siagi mpaka ichanganyike.
3. Mimina
mayai na maziwa uchanganye vizuri.
4. Mimina
Baking Powder kwenye unga na uchanganye vitu vyote pamoja na arki rose.
5. Endelea
kuchanganya vizuri mpaka uhakikishe vimechanganyika vizuri (unaweza kufanya
bila ya mashine)
6. Chukua
trey yenye umbo upendalo ambayo haitojaa
ukiimimina, ipake siagi na umimine mchanganyiko wako. Trey isiwe nzito sana au
nyepesi sana bali iwe wastani.
7. Ipike
(Bake ) mpaka iwive.kama unatumia mkaa moto chini kiasi na juu kiasi ili
isiungue.
8. Epua
iache ipoe ndio ukate kate vipande.
No comments:
Post a Comment